SuccessLiving ni kampeni ilioanzishwa tangu mwaka
2012 nchini Afrika ya kusini kwa ajili ya lengo la kusaidia waafrika kupambana
na umaskini. Kampeni hii ya SuccessLiving
Africa inasimamiwa na taasisi washirika mbalimbali ambao huendesha shule
kadha wa kadha katika nchi kama Afrika ya kusini, Botswana, Zambia, Congo
Brazzaville, Kenya na sasa Tanzania.
Lengo la SuccessLiving ni nini?
Lengo
kuu la kampeni hii, SuccessLiving Afrika, ni kuifanya Afrika sehemu salama ya
kuishi. Kampeni inaendesha shule mbali mbali zinazofundisha njia mbalimbali
zinazoweza kutumika kupambana na umaskini, njia kuu ambayo imependekezwa na
watu wengi katika nchi zilizotembelewa ni ‘biashara’. Biashara ndogo ndogo kwa
kubwa, SuccessLiving inafundisha na kuhakikisha mlengwa anaondokana nao.
SuccessLiving wanafanyeje kazi?
SuccessLiving
Africa inaendesha masomo ya kibiashara kwa wanachama tu. Hii itasaidia
waendeshaji wa kampeni kuwa karibu zaidi na walengwa pia kuhakikisha walengwa
wanapata msaada uliokamilika kuwasaidia kuondokana na umaskini. Ni rahisi kuwa
mwanachama, fomu imeambatanishwa.
Faida za uanachama ni zipi?
Kila
mwanachama atasaidiwa kikamilifu kuondokana na umaskini na walimu waliobobea
katika fani ya biashara pia maendeleo vijijini. Kama mwanachama, utakua na
uwezo wa kuomba msaada wa kiushauri, kimkopo ama kiutendaji kwa walimu wako
popote pale
nchini kwani uanachama wako utakua ki-elektroniki. Kama mwanachama utapewa
kitambulisho ambacho kitakuruhusu kuingia katika darasa lolote la mafunzo
linalosimamiwa na SuccessLiving pia kitakua na namba ambao itasajiliwa
ki-electroniki kumruhusu mwanachama kutambulika popote pale nchini.
![]() |
| Nimechagua SuccessLiving, Naishi na maendeleo pia mafanikio. Jiunge nami leo ujionee mwenyewe. |
Kampeni hii imesaidia watu wengi sana katika nchi zilizotembelewa na kampeni hii, sasa ni wakati wako wewe kubadilisha maisha yako. Jiunge nasi leo!!


